Jumapili, 21 Julai 2019

UMHIMU WA KUNAWA MIKONO NA SABUNI $FAIDA YAKE.


Nikiwa nimeketi mkononi nimeshika
kitafunwa nilichokarimiwa tayari kuanza
kula nikainua macho na kuangalia mbele
yangu na ghafla nikakutana na maandishi
kwenye kioo cha kompyuta yakihamasisha
Ongeza ufahamu kuhusu faida za kunawa mikono kwa sabuni

Maandishi hayo yakanigusa na
kunikumbusha kuwa nilipokea kile kitafunwa nikala bila kunawa mikono zaidi yakanikumbusha kuwa Oktoba 15 ilikuwa,
Siku ya Kimataifa ya Kunawa Mikono kwa Kiingereza, 'Global Handwashing Day'.
Ilinitia aibu nikaenda kutimiza kanuni ya afya kwa kunawa mikono kwa maji safi na sabuni kabla ya kula, kisha nikaendelea na
mlo wangu huku nikiwaza na kupata
msukumo wa kuandika maelezo  ili
kukumbushana umuhimu wa kunawa mikono kabla ya kula.

Sihivyotu bali pia kufanya hivyo kwa majisafi na sabuni baada ya kutoka chooni ili
kuepuka maambukzi ya vimelea vya maradhi
hatari kwa afya zetu.

Vimelea hivi huwapo kwenye mikono ambayo haikusafishwa kwa maji safi na
sabuni na huingia mwilini kila tunapokula,
Bila kunawa kwa maji safi na sabuni Siku hii hukumbukwa kila Oktoba 15 kwa
lengo la kuhamasisha kujenga kwa utamaduni wa kunawa mikono kwa sabuni,
Kwa kila taifa ulimwenguni pia kujua faida zake Kimsingi  siku hiyo  ilianzishwa kwa ajili ya
kuwajengea watoto na wanafunzi na watu wazima
utamaduni wa kunawa mikono,
Inaweza kuadhimishwa na mtu yeyote ndiyo maana inagusa kila jamii
kuiadhimisha kwa kila mtunikikukumbusha
wewe yule na wote manufaa na umuhimu wake katika kunawa mikono kwa maji safi na sabuni,

Takwimu zinaonyesha kuwa karibu watu 200 milioni katika nchi takriban 100 duniani hushiriki katika siku hii muhimu kiafya.
Serikali, mashirika ya kimataifa taasisi za kijamii, kampuni, mashirika yasiyo ya kiserikali na kila mmoja wetu anawajibika
pia kushiriki na kuhamasisha kunawa mikono kwa maji safi na sabuni,
Pamoja na wajibu huu unaweza kujiuliza kwa nini kunawa mikono kwa sabuni?
Kiafya kunawa mikono kwa sabuni ndiyo njia sahihi na nafuu ya kuzuia magonjwa ya
tumbo, kuhara yanayoathiri na kugharimu
maisha ya mamilioni ya watu hasa watoto katika nchi zinazoendelea kila mwaka.

Hali hiyo inamfanya kila mmoja wetu kuwajibika kwa namna moja au nyingine na vifo vya watoto wetu ambao ni taifa la
kesho, Wanaopoteza maisha kwa magonjwa yanayotokana eti na sababu ya kutonawa
mikono kwa sabuni tu.

Ni muhimu tukakumbuka jukumu muhimu katika maisha la kulinda familia zetu hasa
watoto wetu dhidi ya maradhi hata vifo
vinavyotokana na magonjwa ya uambukizo yanayowapata kwa kutonawa mikono kwa
maji safi na sabuni.

Katika hali ya kawaida, inawezekana
kunawa mikono kwa maji safi na sabuni ni zoezi gumu linalohitaji muda mrefu kujizoesha. Pia ikawa ni vigumu kuueneza
utamaduni huo wa kunawa mikono kwa
maji safi na sabuni, lakini tufanye hivyo kwa umuhimu wa kuokoa maisha ya watoto
yasipotee.
Kunawa mikono kwa maji safi na sabuni kabla ya kula na baada ya kutoka chooni ni
utamaduni unaowezekana kujengeka
miongoni mwetu na unaweza kusaidia kwa
kiasi kikubwa kuokoa maisha yetu kuliko kinga ya dawa. Kitaalamu, Tabia hii inaelezwa kuweza kusaidia kupunguza
nusu ya vifo vinavyotokana na magonjwa ya kuhara na robo ya vifo kutokana na magonjwa ya tumbo.
Tufungue milango ya fahamu na kutambua
kwamba tukiwafundisha zaidi watoto wetu tabia hii njema ya kunawa mikono kwa maji safi na sabuni kabla ya kula na baada ya kutoka chooni kutasaidia siyo tu kupunguza idadi ya vifo na maradhi bali tunaweza
kujenga jamii ya ustaarabu.
Maoni yako ni mhimu sana hapa chini na sisi tutayafanyia kazi tunapenda sana ushauri wako.

Jumanne, 16 Julai 2019

.MAFUNZO YA UJASIRIAMALI.

FOMU YA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

ABIOLA SOLIDARITY GROUP
  SLP TEMEKE YOMBO ABIOLA 
   TEL 0759 408 410
           0718 916 282
           0743 788 246
FOMU YA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI 
                SEHEMU YA KWANZA 
                  MAELEZO BINAFSI

JINA ...............
BARUA PEPE.......
BARABARA..........MTAA
WILAYA .........MKOA 

SEHEMU YA PILI

AINA YA MAFUNZO YANAYOFUNDISHWA

A: SABUNI ZA VIPANDE
i Sabuni ya kipande ya kufulia Tsh 60,000
ii Sabuni ya kipande ya kuongea Tsh60,000
iii Sabuni ya kiapnde tiba tsh60,000
sabuni za unga za kufulia Tsh1,000,000

SEHEMU YA PILI
B: SABUNI ZA MAJI
i Sabuni ya maji ya kufulia Tsh40,000
ii Sabuni ya kunawia mikono Tsh40,000
iii Sabuni ya kuoshea nywele(shampoo)Tsh40,000
iv Sabuni ya safishia marumaru(masink)Tsh40,000
v Sabuni ya kuuwa waduduTsh50,000

SEHEMU YA TATU 
C:
USINDIKAJI 
i Kusindika mboga Tsh50,000
ii Kusindika achali ya Embe Tsh 40,000
iii Kusindika siangi ya karanga Tsh40,000
iv Kusindika matunda Tsh60,000
v Kusindka Tomato souse,Mango na piko Tsh100,000 
vi Kusindika chilly souse Tsh100,000
vii Ubuyu wa zanzibar Tsh50,000
vii Ubuyu mtamu wa kashata na pilipili Tsh50,000

SESHEMU YA NNE D.
i Kutengeneza biscuit za chocolate Tsh50,000
ii Kutengeneza pipi toffi Tsh50,000
iii Kutengeneza pipi kijiti Tsh50,000
iv Kutengeneza pipi kifua Tsh50,000
v Kutengeneza cake Tsh100,000

SEHEMU YA TANO E.

MASOMO YA KONI NA ICE CREAM
i Ice cream ya chocolate 
ii Ice cream ya Embe 
iii Ice cream ya maziwa 
iv Ice cream ya ukwaju 
{TSH50,000}

SEHEMU YA SITA F.
MIKOBA 
i Pochi kubwa 
ii wallet               {TSH70,000}

SEHEMU YA SABA G 
BATIKI AINA ZOTE

i Batiki za maua Tsh150,000
ii Batiki za kuprint Tsh 100,000

SEHEMU YA NANE H.
MAFUNZO YA LOTION

i Lotion ya kawaida Tsh50,000
ii  Lotion ya tiba Tsh 50,000
iio Lotion ya kuwa mweupe Tsh50,000

SEHEMU YA TISA I.
MAFUNZO YA NGOZI

i Viatu vya ngozi kiume na kike Tsh 250,000
ii Viatu vya kimasai Tsh250,000

SEHEMU YA 10

KUPAMBA KUMBI ZA SHEREHE 
MAPAMBO AINA 10 TSH 250,000

KARIBU SANA SOLIDARITY

SOLIDARITY NI KIWANDA.

Jumatatu, 15 Julai 2019

NJINSI YA KUADAA PLANI YA BIASHARA YAKO

Jinsi ya kuandaa mpango wa Biashara

Biashara zote nzuri zinahitaji mpangilio. Panga vyema na utatengeneza pesa zaidi. Mpangilio wa biashara unakufanya uangazie malengo yako makuu. Unakutaarifu ulikotoka, umefikia wapi kwa sasa, na ni wapi unahitaji kuenda kama biashara.

Inaweza pia kukusaidia kupata mkopo kutoka benki, inasaidia watu kukukopesha pesa na inawaeleza watu unataka biashara yako iwe vipi katika muda wa miaka 3 mpaka 5.

Hatua ya 1: Muhtasari na maelezo ya biashara

Moja ya vitu vya kwanza unachohitaji kufanya ni kuandika muhtasari wa biashara na maelezo. Hii itakusaidia wewe na wengine kuelewa nini unachotarajia kufanikisha:

Muhtasari wa Biashara: Nini unataka kufanya? Wapi? Vipi? Kwa kiasi gani?Maelezo ya Biashara: Nini kinatokea leo? Nini kinaweza kutokea hapo mbeleni katika eneo lako? Unaweza kufanya nini? Unaweza kuifanya vipi? Kitatengeneza vipi pesa?

Hatua ya 2: Mpango wa uzalishaji

Hakikisha muda wote una kitu cha kuuza kwa mfano ng’ombe wa maziwa. Kama ng’ombe wako wote watazaa kwa wakati moja, hautakua na maziwa ya kuuza. Kama una ng’ombe mmoja anaetoa maziwa, nini kitatokea kama akiwa mgonjwa?

Mara nyingine ni vizuri kuwa na biashara zaidi ya moja. Jaribu kufuga kuku au kupanda mboga au kulima pamba

Hatua ya 3: Mpango wa Masoko

Angalia soko. Nini kinatokea katika soko kwaajili ya biashara yako leo? Hatua muhimu ni kutambua mnunuzi kwaajili ya zao lako, kuhakikisha unahudumia kuendana na mahitaji. Hii itahakikisha unapata rejesho katika uwekezaji wako.

Kuna Ushindani gani hapo? Kama una mshindani, unahitaji kufikiria jinsi unavyoweza kuwa tofauti na kutoa thamani nzuri kwa wateja wako. Utafanya nini kama mshindani akitokea?

Zingatia P 4 zifuatazo – Bei, Bidhaa, Ukuzaji na Mahali:

Uza kwa bei nzuri. Tambua kiasi majirani zako wanachouzia maziwa. Kama bei iko juu sana watu hawatanunua maziwa yako.Bidhaa yako ni gani? Katika hili je maziwa ni safi na mabichi( Haijakaa).Watu wanajuaje kama unauza maziwa? Unahitaji kutangaza . Bango/ Tangazo mlangoni? Kuwajulisha watu kanisani?Wapi watu wanaweza kununua maziwa yako? Nyumbani kwako? Unapeleka? Kwenye OLX au mtandao wa kijamii?

Kwa taarifa zaidi kuhusu kujua masoko bonyeza hapa.

Hatua ya 4: Mpango wa kifedha
 Uzalishaji na utafutaji masoko unagharimu pesa. Unahitaji kiasi gani cha fedha? Je utahitaji mkopo? Una akiba ambazo unaweza kutumia?

Utahitaji kuandaa bajeti. Panga bajeti yako kukopa, kuweka akiba, kuwa na pesa za kuendesha na kukuza biashara yako, na kiasi gani unaweza kujilipa.

Hatua ya 5: Mpango wa kuendesha biashara

Jinsi gani biashara itaendeshwa siku baada ya siku? Je utahitaji watu wa kukusaidia? Je utahitaji kufanyia ukarabati vifaa vyako na je unahitaji usafiri?

Hatua ya 6: Mkadirio ya hatari

Matatizo inaweza kutokea wapi? Ni muhimu kuwaza kwa kinga kuhusu hatari , kwa mfano; Utafanya nini kama mavuno ya mazao yako ni mabaya na kama ng’ombe wako akiwa mgonjwa.
ABIOLA SOLIDARITY NI MATAZAMIO YA KUANZISHA KIWANDA.

FUMO


FOMU YA UWANACHAMA


ABIOLA SOLIDARITY GROUP

PHONE NUMBER; 0759 408 410/0763 812 965

1. TAARIFA YA MWANACHAMA

Jina kamili ;……………………………………………………………….         Jinsia …………………………..……

Tarehe ya kuzaliwa ………………………………… Mahali ulipo……………………………………………....

Utaifa ……………………………… Namba ya kitambulisho cha utaifa …………………………………..

Namba ya simu ……………………………………


Mwanafunzi                     Mfanyabiashara                        Mfanyakazi  

Chuo gani ………………..……   Aina ya biashara ………………..……  Nafasi ya kazi ……………….……


2. TAARIFA YA MTU WA KARIBU

Jina kamili ………………………………………………………………. Jinsia ……………………………………………

Mahali ………………………………. Uhusiano ………………….. Namba ya simu ……………………………


3. TAARIFA YA NJE YA KIKUNDI

Jina la kikundi ………………………………………..   Shughuli za Kikundi ………………………………………

Jina la kiongozi ………………………………………………….. Namba yake ya simu …………………………


4. MALIPO

Nimelipa                                                                                  Sijalipa                

Kiasi ………………………..                                                           Tarehe ya malipo ……………………….

Njia uliyotumia kulipa ………………………                              Njia ya malipo …………………………..

Namba ya risiti ……………………….                                         Namba ya malipo ……………………..


5. MAKUBALIANO

Mimi ………………………………………. Nimekubali kwa hiari yangu kujiunga na kikundi cha Abiola Solidarity Group. Nitafuata taratibu na sharia zote zilizowekwa na umoja huu wa ASG.  Sahihi .............

..

6. UKAGUZI WA FOMU (Matumizi ya ofisi tu)

Jina  …………………………………………………… (Mwenyekiti/Katibu)  Sahihi ………..…………

Jina la muhasibu………………………………………….            Sahihi ………………………....

Jumapili, 14 Julai 2019

HATUA ZA KUTENGENEZA SABUNI YA MAGADI

SABUNI YA MAGADI
malighafi zake
-magadi soda
-mafuta mawese,mbosa
-maji
-rangi
-sodium silicate
-caustic soda

JINSI YA KUTENGENEZA

HATUA 1
-loweka caustic soda kwenye maji lita 5,koroga kwa dakika 15 na acha muda wa siku 7
-siku ƴ ya saba fuata mpangilio huu.chukua caustic soda changanya na magadi  soda 1/2kg loweka na maji lita 1 , koroga kwa dakk 5 halafu changanya na mafuta lita 10,Glycerin 1/2glass,sodium silicate 1/2kg.

Mkorogo wako ukiwa tayar ugawanye mara mbil(1.weka rang,  2.usiweke rangi)
-unavyopeleka  kwenye mudi ,uweke kudogokidogo ukianza na ule usio na rangi halafu wenye rangi hadi utakapomaliza ili mabaki yaweze kuonekana
NB:  1.caustic lita 1-mafuta lita 2  2.caustic lita 1/2-mafuta lita1

Ijumaa, 12 Julai 2019

ABIOLA SOLIDARITY GROUP BEI ZA BIDHAA ZETU

*Habari mpendwa,Napenda kukukaribisha katika kumuunga  mkono Mh.Raisi wetu Magufuli katika kutimiza kauli ya TANZANIA YA VIWANDA*
NINAUZA SABUNI ZINAZOTENGENEZWA NA *SOLIDARITY GROUP*

 SABUNI ZENYE UBORA MZURI,UJAZO KAMILI, HARUFU YA KUPENDEZA NA INAYODUMU *KARIBU NITAKUUZIA KWA BEI NZURI.*

SABUNI YA *DETTOL*
5 ltrs=13,000 -1lt=3,000
*HII KUNG'ARISHA CHOO,HUUWA VIJIDUDU NA KUKIACHA NA HARUFU NZURI KILA MARA.*

*Washing liquid soap*
 1lt =2000 -5lt=9000
*HII YA MAJI YA KUFULIA.HUNG'ARISHA NGUO NA KUIACHA MIKONO YAKO SALAMA NA HAICHUBUI*

*Dishwash*
1/2 ltr  TSH. 2500
*HII NI MAALUMU KWA KUOSHEA VYOMBO.HUVIPA MNG'AO NA KUONDOA MAFUTA YALIYOGANDA*

*Hair Shampoo*
1 ltr TSH 5,000-1/2 1lt TSH.  2500
*HII HUTAKATISHA NYWELE NA KUZIPA MNG'AO NA HAIKAKAMAZI NYWELE.*


*Sink & Tiles*
1lt.TSH 2000
5lt TSH 10,000
*HII INANG'ARISHA MASINKI NA KUYARUDISHA KATIKA RANGI YAKE YA AWALI.PIA KUNG'ARISHA TILES NA KUZIPA MUONEKANO MZURI.*

*

Hand wash*
500 mls  Tshs 3,000/=
250 mls Tshs 2,000/=
*HII HUSAFISHA MIKONO NA KUIACHA NA HARUFU NZURI.HAICHUBUI MIKONO*.

Shower GEL
1lt TSH.  5000
HII HUTAKATISHA NGOZI NA KUIACHA NYORORO YENYE HARUFU NZURI.*
Facebook
@Abiola_solidarity_Group
Instagram
@Abiola_solidarity_Group
Twitter
@Abiola_solidarity_Group
*Asante Naamini umefurahia bei zetu*
Mawasiliano
0759 408 410
0743 788 246
0753 167754

KUTENGENEZA SUNITAIZER

UTATENGENEZAJE SANITAIZER UKIWA NYUMBANI ILI KUJIKINGA NA CORONA Aina ya kwanza Mahitaji 🔸Vineger chupa nzima 🔸vodkta,au highlife hiz...